Muhtasari huu unatoa taswira fupi ya tathmini ya mchango wa ushirikishwaji wa wananchi katika mifumo badilifu ya utoaji wa huduma za maji safi na maji taka (WATSAN) nchini Tanzania. Tathmini hii imefanyika katika wakati muafaka ambapo pamoja na kuwa na zaidi ya muongo mmoja wa utekelezaji wa maboresho ya sera ya maji, machache yanafahamika kuhusu: Mosi, namna ambavyo wananchi wanashiriki kwenye michakato ya utengenezaji na utekelezaji wa maboresho ya huduma; na Pili: mchango ambao jamii unatoa kwenye utoaji wa huduma husika. Taswira hii inatokana na kitabu kilichojikita kwenye uchunguzi wa kina wa huduma za Maji Safi na Maji Taka uliofanyika katika kata ya Kawe, manispaa ya Kinondoni, nchini Tanzania. Utafiti ulitumia fasihi na maandishi mbali mbali kuhusu maboresho ya utumishi wa umma, ushirikishaji wa wananchi na nadharia ya kihistoria ya mfumo wa kitaasisi, katika kuwasilisha na kuchambua kwa kina utekelezaji wa dhana na sera ya ushirikishwaji wa wananchi, mahusiano kati ya watendaji wa kitaasisi na wananchi kwenye utengenezaji na utekelezaji wa maboresho ya sera utoaji wa huduma za maji safi na maji taka katika eneo la tafiti husika.
Related Articles
Unlocking Tanzania’s potential: Youth look to jobs, entrepreneurial opportunities
On their top priorities for government action – including health, water supply, infrastructure/roads, electricity, education, and job creation – young citizens give the government positive performance reviews, and a majority see the country as moving in “the right direction.” But their assessments of economic and living conditions are less positive, and economic opportunity tops of […]
Tanzanians applaud government performance on health, but it remains their top concern
This dispatch/ policy brief presents findings from a special Afrobarometer Round 10 survey module focusing on health care. READ ON by clicking the Download.PDF button…!
Why property tax reforms fail: Lessons from Tanzania
Over the past two decades, property tax administration in Tanzania has undergone substantial changes, shifting between decentralized and centralized collection models. However, despite numerous reform initiatives, these efforts have largely failed to boost tax revenues and improve property tax administration. This CMI (in collaboration with REPOA) Insight outlines five reasons why these reforms have not […]
Strengthening Decentralisation and Local Economic Development in Tanzania: Challenges and Opportunities
The research on decentralisation and Local Economic Development (LED) in Tanzania reveals several key challenges and opportunities. One major challenge is the inconsistency between decentralisation goals and actual implementation, where local government authorities (LGAs) often prioritize service delivery over economic development initiatives. The lack of adequate funding, inadequate capacity among local officials, and insufficient coordination […]