Historia ya sera nchini Tanzania imekuwa ni ya mabadiliko ya mara kwa mara ambayo lengo lake limekuwa ni kuongeza ufanisi na uzalishaji katika sekta muhimu za uchumi. Dokezo hili linatoa muhtasari wa kitabu kilichotokana na utafiti uliochunguza uwezo wa mabadiliko mbali mbali ya sera kuiongezea sekta ya kilimo, hususan wakulima wadogo, nguvu ya ushindani katika masoko mbali mbali ndani na nje ya Tanzania. Ushahidi utokanao na utafiti huu unaonyesha kwamba baadhi ya sera za kilimo zilizotungwa na kutekelezwa mara tu baada ya uhuru zilichangia kuzorotesha uzalishaji wa mazao ya biashara. Unaonyesha pia kwamba sera zilizolenga marekebisho ya kimuundo maarufu kama ‘structural adjustment’ na utandawazi hazikufanikiwa sana kuongeza uzalishaji kwenye kilimo kama ilivyotarajiwa. Kutokana na hilo hoja kubwa ni kwamba ili kuviondoa vikwazo hasi vya kisera kwenye mfumo wa soko vinavyopunguza ufanisi kwenye sekta ya wakulima wadogo, ni vizuri kutumia taratibu na mifumo ya kimasoko na isiyo ya kimasoko kwa uratibu mzuri wa pamoja.
Related Articles
Does obtaining a lot of schooling guarantee a quick transition to employment? Evidence from TVET graduates in Tanzania
This brief assesses the effect of the length of schooling on how long a Technical and Vocational Education Training (TVET) graduate spends unemployed. The analysis is motivated by observations that despite some 800,000 to 1,000,000 of graduates entering the labour market in Tanzania every year (NBS, 2015), on average the economy creates only about 250,000 […]
Tathmini ya Mfumo wa Kitaasisi wa Maboresho wa Utumishi kwa Umma
Muhtasari huu unatoa taswira fupi ya tathmini ya mchango wa ushirikishwaji wa wananchi katika mifumo badilifu ya utoaji wa huduma za maji safi na maji taka (WATSAN) nchini Tanzania. Tathmini hii imefanyika katika wakati muafaka ambapo pamoja na kuwa na zaidi ya muongo mmoja wa utekelezaji wa maboresho ya sera ya maji, machache yanafahamika kuhusu: […]
Institutional Innovations and Barriers to Competitiveness
Case Studies of Smallholder Farmers in Tanzania Tanzania’s policy path has been characterized by institutional reforms aimed at increasing efficiency and productivity in key sectors of the economy. This brief examines the potential of various forms of institutional innovations in building competitiveness of smallholder agriculture in Tanzania. Evidence used shows that while some policies and […]
Elimu na Uzalishaji Kwenye Kilimo Tanzania Vijijini
Hii ni taarifa fupi itokanayo na utafiti wa kitaalam kuhusu mchango wa mfumo rasmi na usiorasmi wa elimu, na upatikanaji wa ardhi na mikopo kwa uzalishaji kwenye kilimo Tanzania katika maeneo ya vijijini. Uchambuzi uliofanywa unasisitiza umuhimu wa elimu rasmi na ile isiyo rasmi, upatikanaji wa ardhi, na uzoefu wa muda mrefu wa stadi za […]